» » Jordan apinga ubaguzi wa rangi Marekani

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Baada ya kipindi cha takribani mwezi, tangu watu weusi kupamba na Polisi nchini, Marekani kwa kile cha kupinga ubaguzi wa rangi, nyota wa zamani wa NBA Michael Jordan, ameahidi kutoa fedha, kuchangia harakati za kukomesha ubaguzi huo.

Gwiji wa mpira wa kikapu, Michael Jordan ameongea kuhusu ubaguzi wa rangi uliopo nchini Marekani sasa hivi na amesema atachangia dola milioni mbili kwa ajili ya kusaidia mahusiano mazuri.

Mchezaji huyo wa zamani wa Chicago Bulls, ambaye alikosolewa kwa ukimya wake kuhusu mambo ya kisiasa wakati alipokuwa bado anacheza mpira wa kikapu, hawezi kuendelea kuwa kimya.

Maneneo ya Jordan, yanakuja baada ya Polisi kuuwa Wamarekani wawili wanaume, wenye asili ya Africa, , Alton Sterling na Philando Castile, kwenye miji ya Dallas na Baton Rouge.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post