» » Wapinga Kisutu kusikiliza kesi yao

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mahakama ya Kisutu. 


Dar es Salaam.  Mawakili wa Mhariri wa gazeti la Mawio, Simon Mkina na wenzake watatu katika kesi ya uchochezi iliyofunguliwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wamepinga korti hiyo kusikiliza shauri hilo kwa madai haina mamlaka kisheria.
 Mkina na wenzake wanakabiliwa na kesi ya uchochezi baada ya kuandika na kuchapisha makala yenye kichwa cha habari “Machafuko yaja Zanzibar” katika gazeti la Mawio la Januari 14-20, mwaka huu.
 Washtakiwa wengine katika kesi hiyo, mbali na Mkina, ni mwandishi wa makala hiyo, Jabir Idrissa ambaye ni mshtakiwa wa kwanza; Ismail Mehboob, ambaye ni mmiliki wa mtambo uliochapisha gazeti lenye makala hiyo, na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post