» » Mahakama Kuu yampa agizo zito AG

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Dar es Salaam. Mahakama Kuu ya Tanzania imemwagiza Mwanasheria Mkuu (AG) kufanya maboresho katika Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) ndani ya miezi sita, ili kuzipatia mahakama za chini nguvu ya kusikiliza makosa makubwa ya jinai na kuwaondolea wananchi kadhia ya kusota rumande.

 Agizo hilo lilitolewa na Mahakama hiyo katika hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Zephrine Galeba dhidi ya AG, aliyetaka Mahakama itamke kuwa vifungu namba 244 na 245 (1) (2) na (3) sura ya 20 iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002, vinakinzana na ibara ya 13 (6) (a) ya Katiba ya mwaka 1977 inayotaka haki na usawa.

Katika kesi hiyo, mwanasheria aliyekuwa akimwakilisha Galeba, Wakili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk James Jesse aliiambia Mahakama kuwa kitendo cha makosa makubwa ya jinai kufunguliwa katika Mahakama zisizo na uwezo huo kinachelewesha haki.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post