» » SAID FELLA NA BABU TALE KUMRUDISHA UPYA MSANII CHID BENZI KWENYE GAME

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

MKURUGENZI wa kundi la Wanaume Family na Yamoto bendi, Saidi Fella maarufu Mkubwa Fella, amesema yeye na meneja wa msanii, Diamond Platnumz, Babu Tale, wameamua kumsaidia mkali wa rapu, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’, arudi katika sanaa yake na si kujiunga na kundi lolote.

Fella alisema msanii huyo kwa sasa wamemwanzishia mazoezi maalumu ya kumwezesha kurudisha mwili wake na pumzi ili aweze kurudisha makali yake katika uimbaji bila kuchoka.
“Chid Benzi hawezi kujiunga na Wasafi kwa sasa mimi na Babu Tale tumekubaliana tumsaidie yeye kama yeye na si kujiunga na kundi lolote lakini kama anataka kujiunga na lebo yoyote hilo litakuwa la kwake,” alifafanua Mkubwa Fella.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post