» » Hali yazidi kuwa tete kitongoji kulikotokea mauaji ya kinyama

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Tanga. Hali imeendelea kuwa tete katika Kitongoji cha Kibatini mkoani Tanga kulikotokea mauaji ya watu wanane waliochinjwa shingo zao.

Wakazi wa eneo hilo wameanza kuyahama makazi yao wakihofia usalama wa maisha yao.

Watu hao walichinjwa usiku wa Mei 31 nje ya nyumba ya mwenyekiti wa kitongoji hicho kwa madai kuwa walisababisha “vijana” wao kukamatwa na polisi baada ya kutoa taarifa zao wakati wakizurura kwenye eneo lao.

Jana baada ya maziko, mbunge wa Tanga Mjini, Mussa Mbarouk alipeleka lori aina ya Mitsubishi Fusso kwa ajili ya kuwahamisha wanakijiji hao.

Diwani wa kata ya Mzizima, Fredrick Chiluba alisema wakazi hao wameamua kuhamia kitongoji cha Kona-Z kilichopo kijiji jirani cha Kiomoni.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post