» »Unlabelled » Wema, Kiba Waangukia Pua Mtandaoni Diamond Awanyoosha

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

MREMBO asiyeishiwa matukio kila kukicha Bongo, Wema Isaac Sepetu na msanii wa Bongo Fleva anayewika kwa wimbo wake Aje, Ali Kiba, mwisho wa wiki hii wamenagukia pua katika mitandao ya kijamii na Diamond Platnumz ameendelea kuwaonyesha kuwa yeye ana nguvu kuwazidi wao mtandaoni.
Wema Sepatu.
Awali iliripotiwa kuwa Wema amefuta picha zake zote katika mtandao wake wa Instagram kwa shabaha ya kurudi kwa kishindo na kuwaonyesha watu kuwa yeye ndiye malkia wa mtandao huo hapa nchini. Jitihada zake ziligonga mwamba pale aliporejea na kutegemea mapokezi makubwa na haikuwa hivyo. Daimond aliweka video ya familia yake iliyowaonyesha laivu akiwa na mkewe na mwanaye Tiffa Dangote.
Daimond na familia yake wakiwa laivu Instagram.
Video hiyo ilipata watazamaji 20,708 na wachangiaji zaidi ya 600 na kusababisha watu wengi kuacha kumzingatia Wema na kurudi kwa Diamond.
Ali Kibba.
Aidha Ali Kiba amekuwa akiendelea kushushiwa matusi na kupewa lawama na mashabiki zake baada ya kuonekana mahojioano kupitia vituo mbalimbali vya televisheni akisema kuwa yeye hapo alipofika ni juhudi zake.
Mashabiki zake hawakupendezwa na kauli hiyo na kuitafsiri kama majigambo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post