» »Unlabelled » Lukuvi awapania viongozi Hawa..

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Iringa. Waziri wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema chanzo cha migogoro inayolikabili Taifa kwa sasa hususan wakulima na wafugaji,  imetokana na kukosekana kwa mipango bora ya matumizi ya ardhi, huku viongozi wa serikali za vijiji wakibadilisha matumizi bila kushirikisha wananchi.
Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi hati 810 za kimila za kumiliki ardhi kwa wakazi wa Kijiji cha Kinywang’anga, Wilaya ya Iringa mkoani hapa.
 “Tumejifunza kutokana na uzoefu tuliopata, migogoro mingi ya ardhi imetokana na baadhi ya  viongozi wetu wa serikali za vijiji ambao wamekuwa wakibadilisha matumizi ya ardhi bila kufuata utaratibu,” alisema.
Lukuvi alisema Serikali haitasita kuwafuta kazi viongozi  wa serikali za vijiji watakaobainika kujihusisha kubadili  mpango wa matumizi bora ya ardhi za vijiji bila ya kushirikisha wananchi.
Alisema licha ya kuwaondoa kwenye nafasi zao, viongozi hao watakamatwa na kufikishwa katika  vyombo vya sheria kwa tuhuma za matumizi mabaya  ya madaraka.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Msaidizi wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID),  Dan Thompson alisema wanaendesha miradi ya aina hiyo kwenye vijiji 41 vya mikoa ya Iringa na Mbeya kupitia Mradi wa Feed the Future.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post