» »Unlabelled » Kupoteza muda kulalamika MAISHA NI MAGUMU hakutayabadilisha,FANYA HIVI

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Usitegemee ipo siku Serikali itaanza kugawa hela ili maisha yawe RAHISI.Never,Tangu enzi za Mwalimu mpaka enzi za Jakaya kuna watu wamekuwa wakilalamika MAISHA NI MAGUMU lakini katika hayohayo maisha magumu MATAJIRI WALIKUWEPO na hata sasa MATAJIRI WAPO.

Kupoteza muda kulalamika MAISHA NI MAGUMU hakutayabadilisha yawe rahisi Kitakachobadili kauli hii ni WEWE KUBADILIKA. Maisha hayatabadilika kamwe kama wewe hubadiliki.Unaishi maisha yaleyale,Una marafiki walewale,Unaishi kwa mbinu zilezile halafu unategemea Maisha yatabadilika (LIFE WILL CHANGE).How,kwa MAGAZIJUTO au??

Wenzio kila siku wanafanikiwa kimaisha wewe unabaki unatumbua macho tu kama umefumaniwa na mke wa Askari wa BOKOHARAM, siku zote maisha yataendelea kuwa magumu kama utokuwa jasiri kukabiliana nayo (Life will always be tough if you are not TOUGHER enough to challenge it. Kuwa Jasiri  mpaka Maisha yenyewe yakikuona umeamka asubuhi yajue THE TROUBLEMAKER IS AWAKE!

Kuna wakati hapa juzi nilijihisi NINA VITU VINGI SANA nafanya mpaka nilipokaa na Mzee mmoja ambaye ameoa, he is over 50 years na ameajiriwa akanifungukia kwenye mfuko kwa kuniambia mambo anayofanya,NIKASEMA SHIKAMOO,kumbe mimi bado sana ana ajira inayomfanya awe bize kama wengi wetu humu. Anafuga Nyuki wa Asali,nafuga Samaki,Analima Mahindi, Ana mashamba ya Alizeti,Analisha Chakula,Ana tenda za kwenye Meli na Anafanya Cleaning service.

Niliondoka ofisini kwake kwa hasira isiyo mfano nikasema kumbe bado nIna mengi ya kufanya.

Swali la kujiuliza je wewe una VITEGA UCHUMI VINGAPI (REVENUE STREAMS) ? Unalala kutegemea Mshahara tu ambao unalipwa nakusuburi nyingine PPF? Wenzio wana Mirija 10 ya Kuingiza hela mwisho kwa mwezi na wanazidi kuwekeza zaidi,Sawa Maisha ni Magumu, JE UMEFANYA JITIHADA GANI KUYALAINISHA,Tangu uanze kulalamika Maisha Magumu umeongeza shi'ngapi kwenye akiba yako? CHANGE YOUR LIFE OR DIE,kelele hazisaidii,NDIYO MAISHA NI MAGUMU TENA MAGUMU SANA LAKINI SIYO KWA WATU WOTE kwanini wewe usiwe kwenye hilo kundi ambalo si la watu wote.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post