» »Unlabelled » WAKAZI wa Mtaa wa Kunguru, waomba kubadilishiwa jina hilo

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Tuesday, December 13, 2016

WAKAZI wa Mtaa wa Kunguru, Kata ya Goba, Manispaa ya Ubungo, Dar es Salaam wameomba mamlaka kuwabadilishia jina la mtaa wao kwani lililopo haliwafai.

Tokeo la picha la wakazi wa goba

Wakizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wa wananchi na Kampuni ya Upangaji na Upimaji Makazi (HUSEA), uliofanyika Shule ya Upili ya Mtakatifu Joseph iliyopo Goba, wakazi hao walisema jina la Kunguru na tabia ya ndege huyo za wizi na uchafu, linaupa taswira mbaya mtaa wao.

Kilio cha wananchi hao pia kilisikilizwa na Meya wa Ubungo, Boniface Jacob aliyetakiwa awasaidie kubadilisha jina hilo. Hata hivyo wananchi hao hawakutaja jina jipya ambalo wanalitaka.

Akitolea ufafanuzi suala hilo, Meya Jacob alisema hakuna ugumu kwenye kubadili jina ikiwa wengi wataridhia, huku akiwapa utaratibu wa kufuata waweze kutimiza matakwa yao.

Alisema wanachotakiwa kukifanya ni kukusanya sahihi zisizopungua nusu ya wakazi wa mtaa mzima na waandike barua kwa halmashauri kuomba kubadilisha jina na kutaja jipya wanalolipendekeza.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post