» »Unlabelled » Pacha walioshikana kichwani watenganishwa New York

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Hali kama hiyo hutokea katika mtoto mmoja kati ya 10 milioni wanaozaliwa

Wavulana wawili pacha ambao walikuwa wameshikana vichwani wametenganishwa na madaktari mjini New York, Marekani.

Jadon na Anias McDonald wa umri wa miezi 13 walifanyiwa upasuaji uliochukua saa 16 katika hospitali ya Montefiore.

Kwa sasa wanafanyiwa matibabu ya kuwezesha mafuvu ya vichwa vyao kukua na kujaza pengo lililoachwa.

Mama yao Nicole McDonald aliandika kwenye Facebook Ijumaa asubuhi jinsi alivyokuwa na furaha lakini pia na "uchungu kuhusu mustakabali wa watoto hao."

Alipakia picha ya Jadon akiwa peke yake kitandani.

"Hata niliwauliza mbona walipanga upya chumba cha kulala kwa sababu haikuwa imeniingia akilini kwamba ningehitaji kitanda cha ziada," Bi McDonald aliandika.

Alisema wasichana hao ni kama wamezaliwa upya.
Madaktari wanasema wavulana hao watalishwa kwa kutumia mifereji kwa kutumia neli (tyubu) kwa wiki moja zaidi

Wavulana hao walizaliwa wakiwa na mishipa ya damu na sehemu za ubongo zilizoshikana, tatizo ambalo hutokea katika kisa kimoja kati ya visa 10 milioni vya kuzaliwa kwa watoto.

Familia ya McDonald ilikuwa imechangisha $100,000 kugharimia upasuaji huo.

Dkt James Goodrich, aliyekuwa amefanya upasuaji sawa kwa watoto wengine wakiwepo pacha kutoka Syria mapema mwaka huu alijiandaa kwa upasuaji huo kwa kutumia mfano wa 3D.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post