» »Unlabelled » Mama Magufuli aonya wanaotafuna misaada ya wazee

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli (Kushoto),akimsalimia mmoja ya wazee walio katika kituo cha kulelea wazee.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha kuwa wazee na watu wenye ulemavu wanapata huduma za kijamii haraka iwezekanavyo.

Mama Magufuli amesema hayo mara baada ya kutembelea Kituo cha kulelea wazee cha Funga Funga kilichopo Morogoro mjini, na kutoa msaada wa chakula ukiwemo unga kilo 1300, mchele kilo 1300, maharage kilo 570, mafuta ya alizeti lita 260, sukari kilo 260 pamoja na boksi moja la mafuta kwa wazee wenye ualbino.

Aidha amewaomba watumishi wa kituo hicho kukitumia vizuri chakula hicho, kutokana na viongozi wengine ambao ni watumishi wa vituo kama hicho, kutokuwa waadilifu, kutokana na kuuza chakula cha msaada unaotolewa kwa ajili ya kuwasaidia wazee wenye uhitaji.

Hata hivyo amewashukuru wadau mbambali ambao wamejitolea, kuwachangia wazee hao, huku akiziomba taasisi za serikali, mashirika ya watu binafsi, na watu wote wenye mapenzi mema kujitahidi kuwasaidia wazee.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post