» »Unlabelled » Dereva, Utingo wadakwa na mirungi

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Moshi. Dereva wa lori aina ya Mitsubish Fusso na utingo wake wamefikishwa mahakamani wakidaiwa kusafirisha kilo 346.58 za dawa za kulevya aina ya mirungi.

Waliofikishwa  mbele ya Hakimu Mkazi, Pamela Meena ni dereva Ally Msangi (26), utingo Rashid Salim (22) na Hamza Juma (22) ambaye ni mkulima.

Wakili wa Serikali, Agatha Pima, akiwasomea mashtaka alidai Septemba 28, katika barabara ya Holili-Himo walisafirisha dawa hizo.

Washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kusikiliza shauri hilo bali Mahakama Kuu. Kesi imepangwa kutajwa Oktoba 25.

Kwa mujibu wa Sheria ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya ya mwaka 2015, shtaka linalowakabili washtakiwa hao halina dhamana kama ilivyo kwa makosa ya mauaji, wizi wa kutumia silaha na uhaini.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post