» »Unlabelled » Akamatwa kwa madai ya kumnyonga mwanaye

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Kibiti. Jeshi la Polisi mkoani Pwani linamshikilia mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Mariam Haji mkazi wa Kitongoji cha Mbebetini wilayani Kibiti mkoani Pwani kwa tuhuma za kumnyonga mwanaye hadi kufa kisha kuutupa mwili wa marehemu kwenye kisima chenye maji.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Bonaventure Mushongi alisema mwanamke huyo alitumia kamba ya kitambaa kumnyonga mwanaye Majaliwa Muhidini mwenye mwezi mmoja hadi kufa.

Alisema mwanamke huyo baada ya kutekeleza mauaji hayo alikwenda kuutupa mwili wa mtoto huyo kwenye kisima cha maji.

Alisema kutokana na tukio hilo jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi dhidi ya tukio hilo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post