» »Unlabelled » Fidel Castro wa Cuba atimiza miaka 90

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Kiongozi mwanamapinduzi wa Cuba Fidel Castro anasherehekea kutimiza miaka 90 tangu kuzaliwa kwake.

Mzee huyo, aliyetawala kisiwa hicho kwa zaidi ya miaka 50, hajaonekana hadharani kwa miezi mingi na bado haijabainika iwapo atajitokeza leo.

Ingawa Cuba imebadilika sana tangu kakake Raul achukue hatamu miaka minane iliyopita, na ushawishi wa Fidel umeshuka, bado anaenziwa sana na raia wengi wa Cuba.

Hakuna hafla yoyote rasmi iliyopangiwa kufanywa, lakini Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, taifa mshirika wa karibu wa Cuba, amewasili Havana kushiriki katika sherehe hizo.

Mtengenezaji sigara maarufu raia wa Cuba ametayarisha msokoto mrefu zaidi wa sigara duniani kwa heshima ya Castro.

Msokoto huo una urefu wa mita 90.

Source: BBC
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post