Mkongwe Dully Sykes alishikwa mkono na kijana wa WCB, Harmonize ambaye label yake iligharamikia kila kitu kwenye mradi wake mpya, Inde.
Akiongea na Clouds E ya Clouds TV, Dully alidai kuwa Inde ni zawadi aliyopewa na WCB kama kumlipa fadhila ya jinsi alivyokuwa msaada mkubwa kwa Diamond na wasanii wengine wa label hiyo. Amedai kuwa hakuwa na mpango wa kuachia ngoma mpya hadi mwakani.
Staa huyo ameongeza kuwa pamoja na kuwa ni producer na mmiliki wa studio yake mwenyewe, aliamua kuacha Inde ifanywe kwenye studio za WCB ili kupata ladha mpya.
Hata hivyo aliongeza kuwa ni yeye ndiye alimpa wazo Diamond la kuanzisha studio yake mwenyewe na kwamba anafurahi kuona kuwa wazo hilo lilifanyiwa kazi na limezaa matunda.
Akiongea na Clouds E ya Clouds TV, Dully alidai kuwa Inde ni zawadi aliyopewa na WCB kama kumlipa fadhila ya jinsi alivyokuwa msaada mkubwa kwa Diamond na wasanii wengine wa label hiyo. Amedai kuwa hakuwa na mpango wa kuachia ngoma mpya hadi mwakani.
Staa huyo ameongeza kuwa pamoja na kuwa ni producer na mmiliki wa studio yake mwenyewe, aliamua kuacha Inde ifanywe kwenye studio za WCB ili kupata ladha mpya.
Hata hivyo aliongeza kuwa ni yeye ndiye alimpa wazo Diamond la kuanzisha studio yake mwenyewe na kwamba anafurahi kuona kuwa wazo hilo lilifanyiwa kazi na limezaa matunda.
