» » » Zlatan ampokonya namba Anthony Martial

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Namba za awali za wachezaji wa Manchester United kwa ajili ya msimu ujao zimetangazwa. Hii ni habari kubwa kwa sababu kadha wa kadha. Kwa sababu kuna namba ambayo imeachwa wazi, na taarifa za awali zinadai kwamba namba hiyo ipo kwa ajili ya Paul Pogba.

Kingine ni juu ya Zlatan Ibrahimovic, amepewa namba tisa ambayo hapo awali ilikuwa ikitumiwa na Anthony Martial.

Kwa sasa Martial aakuwa akivaa namba saba, huku Adnan Januzaj akipewa namba 15.

Baada ya namba hizo za jezi kutolewa, Zlatan alipost ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika hivi: “Nilichagua namba 9”, hii inaonesha dhahiri kwamba amefurahia kupewa namba hiyo na hatajali kama Martial atakerwa na jambo hilo ama la!

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post