» » Wanasayansi wanaamini maziwa ya mende yatakuwa dili siku za usoni, utayanywa?

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Timu ya kimataifa ya wanasayansi imegundua virutubisho muhimu vya protini kwenye maziwa ya mende – ndiyo mdudu mende usiyempenda kabisa!


Maziwa hayo yana virutubisho mara nne zaidi ya maziwa ya ng’ombe na wanasayansi wamedai kuwa yanaweza kuwa muhimu katika kuwalisha watu wanaongezeka duniani siku za usoni.

Ingawa mende wengi hawatoi maziwa, mende aina ya Diploptera punctate, wameonekana kutoa utomvu unaonekana kama maziwa yenye protini yanayotumika kuwalisha watoto wao.

Ukweli kwamba kumbe wadudu nao hutoa maziwa unastaajabisha lakini kilichowashangaza zaidi watafiti ni kuwa maziwa yao yana nguvu mara tatu zaidi ya ile inayopatikana kwenye maziwa ya kifaru.

Utafiti huo ulifanywa na wanasayansi wa Institute of Stem Cell Biology and Regenerative Medicine ya India.

Soma zaidi habari hii hapa.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post