» » Sport Pesa ya Kenya kuwa mdhamini wa klabu ya Hull City ya Uingereza

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Kampuni ya mashindano ya bahati nasibu inayodhamini Ligi Kuu ya Kenya imetia saini mkataba wa kuwa mdhamini wa klabu ya Hull City ya Uingereza.

160725091236_hull_city_640x360_reuters
Kampuni hiyo ya SportPesa, ambayo huandaa mashindano ya kubashiri matokeo ya mechi nchini Kenya, imetia saini mkataba wa kudhamini Hull City kwa misimu mitatu.
Klabu ya Hull City ilifanikiwa kurejea kwenye Ligi ya Premia msimu utakaoanza mwezi ujao.
Hull City watafungua msimu kwa mechi ya nyumbani dhidi ya mabingwa Leicester City.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa klabu hiyo, udhamini wa SportPesa ndio wa juu zaidi kuwahi kupokelewa na klabu hiyo katika historia yake ya miaka 112.
Hull City imekuwa ikidhaminiwa na kituo cha burudani cha Flamingo Land.
Source: BBC
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post