Mbunge wa Jimbo la Ulanga CCM Goodluck Mlinga.
'Wale vyama vya siasa wanataka kujijenga kisiasa watajijenga kisiasa kwa namna gani , zile tunaziita sanaa za kisiasa, kwa sababu naibu spika amechaguliwa na wengi na wengi ndani ya Bunge ni wabunge wa ccm sasa wangewezaje kumtoa kirahisi na hana mapungufu kama wanavyosema''Amesema Mlinga.
Mlinga ameyasema hayp alipofanya hahojiano na EABreakFast Jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa Bungeni kuna kanuni kama zilivyokuwa sehemu za kazi, Naibu Spika yupo vizuri sana katika kusimamia sheria.
Sababu ambayo waliitaja ya kutoka nje ilikuwa ni wanafunzi wa UDOM kufukuzwa chuo na hata ajenda hiyo ililetwa na wabunge wa CCM kwa hiyo lengo lao ni kujijenga kisiasa.
''Asilimia 99% ya wabunge wa upinzani walikuwa hawapendelei ile hali siyo kwamba sababu ya fedha tuu bali hali ile ilikuwa inawadhalilisha'' ameongeza Mlinga
Bunge la 11 mkutano wa tatu uliomalizika hivi karibuni Mkoani Dodoma wabunge wa upinzani walisusia vikao zaidi ya wiki tatu ambavyo viliongozwa na naibu Spika kwa kusema kwamba hawana imani naye.
