» » Wabunge kususia Bunge ilikuwa sanaa-Mlinga

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mbunge wa Jimbo la Ulanga CCM Goodluck Mlinga.

Mbunge wa Jimbo la Ulanga Goodluck Mlinga amesema kwamba kitendo cha wabunge wa upinzani kususia vikao vya bunge la bajeti lililopita kwa kisingizio cha kutokuwa na imani na Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson ni sanaa ya kisiasa.

'Wale vyama vya siasa wanataka kujijenga kisiasa watajijenga kisiasa kwa namna gani , zile tunaziita sanaa za kisiasa, kwa sababu naibu spika amechaguliwa na wengi na wengi ndani ya Bunge ni wabunge wa ccm sasa wangewezaje kumtoa kirahisi na hana mapungufu kama wanavyosema''Amesema Mlinga.

Mlinga ameyasema hayp alipofanya hahojiano na EABreakFast Jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa Bungeni kuna kanuni kama zilivyokuwa sehemu za kazi, Naibu Spika yupo vizuri sana katika kusimamia sheria.

Sababu ambayo waliitaja ya kutoka nje ilikuwa ni wanafunzi wa UDOM kufukuzwa chuo na hata ajenda hiyo ililetwa na wabunge wa CCM kwa hiyo lengo lao ni kujijenga kisiasa.

''Asilimia 99% ya wabunge wa upinzani walikuwa hawapendelei ile hali siyo kwamba sababu ya fedha tuu bali hali ile ilikuwa inawadhalilisha'' ameongeza Mlinga

Bunge la 11 mkutano wa tatu uliomalizika hivi karibuni Mkoani Dodoma wabunge wa upinzani walisusia vikao zaidi ya wiki tatu ambavyo viliongozwa na naibu Spika kwa kusema kwamba hawana imani naye.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post