» » Sauti yaashiria Juhudi za kujaribu kuuzima moto uliowaka ndani ya ndege

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Sauti iliyorikodiwa kutoka chumba cha rubani cha ndege ya Misri iliyoanguka katika bahari ya Mediterania mwezi Mei, zinaashiria kufanyika kwa juhudi za kujaribu kuuzima moto uliowaka ndani ya ndege hiyo.

Vyanzo vya habari kutoka kamati ya uchunguzi wa ajali hiyo, vimesema sauti hizo zinakwenda sambamba na rekodi za ndani ya ndege hiyo, ambazo awali zilidokeza kwamba moshi ulifuka katika chumba cha kuongozea ndege, na katika vyoo vya ndege hiyo.

Ndege hiyo ya shirika la ndege la Misri, EgyptAir chapa MS804 ilianguka baharini tarehe 19 Mei ikiwa safarini kutoka Paris kwenda Cairo, na kuuwa watu wote 66 waliokuwa ndani yake.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post