» » » Yanga yamaliza kambi Uturuki, yawafuata Waalgeria

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Kikosi cha Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara timu ya Yanga kimeondoka nchini Uturuki kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wao wa kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya Mo Bejaia Juni 19.

Yanga waliweka kambi ya muda mfupi nchini Uturuki kwa ajili ya kuwavutia kasi Waalgeria katika mchezo wa ugenini ambao wanatakiwa kufanya vizuri ili kujiwekea mazingira mazuri katika mechi zake zinazofuata.

Meneja wa Yanga Hafidh Saleh amesema, maandalizi ya mchezo yamekamilika kwa asilimia kubwa na wamefanya mazoezi ya asubuhi, mchana na usiku kwa kuangalia ratiba ya mchezo ambao utachezwa usiku nchini Algeria.

Hafidh amesema, hakuna mchezaji ambaye amepata majeruhi kitu ambacho kinampa kocha kuwa na wigo mpana wa kuchagua nani wa kucheza katika mtanange huo.

Yanga ilikuwa kambini Uturuki kwa siku tano kujiandaa na mechi hiyo ya kwanza ya Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali itakayopigwa Jumapili.

Baada ya mchezo huo Yanga itarejea nyumbani kujiandaa na mchezo dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa Juni 28 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post