Hali hiyo imesababisha watoto wengi kuendelea kufanyiwa ukatili ambapo takwimu zilizotolewa katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika zilizofanyika kata ya Themi zinaonyesha kuwa watoto wengi wanaofanya vitendo hivyo ni wanafamilia na wamekuwa wanaficha ushahidi.
Diwani wa kata ya Themi ambayo ni miongoni mwa zinazotajwa kukithiri kwa ukatili wa watoto Bw Melance Kinabo na baadhi ya viongozi kuna haja ya serikali kuangalia upya namna ya kushughulikia ukatili dhidi ya watoto na jinsi ya kuwapata wanaendesha vitendo hivyo kwani muundo wa sheria zilizopo sasa hivi unaonekana una mapungufu makubwa.
Naibu Meya wa jiji la Arusha Bi Viola Lazaro Meikoki amesema tatizo la watu kuficha ushahidi wa ukatili dhidi ya watoto ni kubwa zaidi kwenye jamii zinazoendelea kudumisha mila na desturi ambazo zinaamini kuwa masuala ya kifamilia yakishughulikiwa na vyombo vya dola husababisha laana.
