» » Wachina waongoza kuingia nchini kinyume cha sheria mwaka huu

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


 

Dar es Salaam. Raia wa China wameelezwa kuongoza kuingia nchini kinyume cha sheria katika kipindi cha miezi minne (Januari mpaka Aprili) wakifuatiwa na Waethiopia.
Naibu Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, Wilson Bambaganya alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano na wanahabari akisema jumla ya wahamiaji haramu 4,792 wamekamatwa nchini katika kipindi hicho.
“Serikali inaandaa mikakati ya kudhibiti na kutambua njia zote za panya (zisizo rasmi) ambazo hutumiwa na wahamiaji haramu kuingia nchini kinyume cha sheria ili kudhibiti tatizo hilo.
Alisema changamoto kubwa katika udhibiti wa wahamiaji haramu ni ukubwa na uwazi wa mipaka yetu sanjari na uwanda mkubwa wa bahari.
“Serikali inafanya jitihada kubwa kuhakikisha tatizo hili linadhibitiwa licha ya kuwapo kwa magari machache ya doria hususani maeneo ya mipakani na boti lakini jitihada zinafanyika kutatua,” alisema Bambaganya.
Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Utawala na Fedha ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Abbas Irovya alisema operesheni ya kuwaondoa wahamiaji haramu nchini imefanikisha kubaini waliokamtwa.
“Wahamiaji 388 walikamatwa na kulipa faini, 509 upelelezi wao bado unaendelea ikiwa ni pamoja na taratibu za kimahakama na kujenga ushahidi,” alisema.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post