
Dar
es Salaam. Kampuni ya UdaRT imeanzisha mfumo mpya wa kadi za
kielekroniki kwa ajili ya malipo ya nauli kwa watumiaji wa usafiri wa
mabasi yaendayo haraka.
Mkurugenzi
mtendaji wa UdaRT, David Mgwassa amesema kadi hizo zitaanza kuuzwa
kesho katika vituo vikuu vya mabasi vya Kimara, Ubungo, Morocco,
Gerezani na Kivukoni.
Kwa
upande wake mkurugenzi wa kampuni ya Maxcom Afrika ambao ndiyo
watengenezaji wa kadi hizo, Juma Rajab amesema bei ya kadi hiyo ni Sh
5,000 na itakuwa na Sh 4,500 ndani yake ambazo abiria anaweza kuzitumia
kama nauli kwa safari nane.
Ameaema kadi hizo hazitakuwa na namba ya siri na kuwa kiwango cha juu kitakachowekwa katika kadi hiyo ni Sh30,000.
