STAA wa Muziki wa Kizazi Kipya,
Snura Mushi ambaye alipata kiki ya aina yake kwa kibao chake cha
Majanga, amefunguka kuwa licha ya kupata shoo nyingi kupitia ngoma hiyo,
lakini pia alipata majanga kwa kutapeliwa mara kadhaa.
Akipiga stori na Risasi Vibes, Snura
alisema promota mmoja alimpeleka kufanya shoo mkoani Kilimanjaro na
Mererani Arusha, lakini baada ya kuwa ameshafanya kazi, mtu huyo
alimkimbia bila kumpa chake, kiasi kwamba alilazimika kurejea Dar kwa
lifti.
“Sitasahau, nilisaidiwa lifti mimi na
wacheza shoo wangu kutuleta Dar, lakini baadaye nilikuja kumpata huyo
promota, nikamnyang’anya pete ya ndoa na uchumba, ninazo mpaka leo maana
hakunilipa,” alisema Snura.
SOURCE:GP