MSANII anayefanya vizuri katika
filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amefungukia hofu aliyonayo kwa mwanaye,
Ipsium kutokana na wanaume wakware kuzidi kuongezeka kila siku.
Akichonga na Risasi Vibes, Nisha alisema
hata akiwa na ‘boyfriend’ wake, huwa hapendi amzoee mwanaye huyo, kwani
anamlea katika maadili ya kidini zaidi na anamshukuru Mungu anazingatia
vile anavyotaka.
“Mwanangu yuko darasa la saba na analala
shuleni lakini wakifunga, huwa anarudi nyumbani hivyo kwa kuwa nasafiri
mara nyingi, huwa nawapeleka yeye na dada wa kazi kwa mama yangu ili
kuepusha wanaume wakware wasiniharibie mwanangu maana nina hofu sana na
wanaume wakware,” alisema Nisha.