Shoo
ya ghafla iliyofanywa na rapa wa Marekani, Kanye West mjini New York,
iliahirishwa baada ya maelfu ya mashabiki kufika eneo la shoo na kuzua
ghasia.
Zaidi ya mashabiki 4000 walifika katika ukumbi wa Webster ulio na uwezo wa kuchukua watu 1500.
Mashabiki walimiminika barabarani na
kisha kupanda juu ya magari wakichungulia kupitia madirisha, angalu
kumuona mwanamuziki huyo.
Kanye alisema kuwa atafanya shoo hiyo ya
ghafla kwenye mitandao ya kijamii baada ile ya mji wa New York kufutwa
kutokana na hali mbaya ya hewa.