» » » Paroko awataka viongozi wastaafu kushauri Bunge

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO



 

Dodoma. Wito umetolewa kwa marais na maspika wastaafu wa Tanzania kusaidia kutoa ushauri wa namna bora ya uendeshaji wa shughuli za vikao vya Bunge kwa sasa, hususani katika kipindi hiki cha vyama vingi ili wananchi waweze kuwakilishwa vyema zaidi kuhusu mahitaji yao bungeni.
Pia, Watanzania wametakiwa kufanya maombi maalumu yenye lengo la kuliombea Bunge ili liweze kurudi katika misingi ya awali kwa kujenga umoja, mshikamano na uvumilivu wakati wa vikao na kuweka mbele dhamira ya ya kuwawakilisha wananchi.
Wito huo umetolewa na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mt Paulo wa Msalaba la mjini Dodoma, Padri Sebastian Mwaja wakati wa mahubiri ya ibada iliyofanyika kanisani hapo.
“Bunge la sasa linaloendelea na vikao vyake hapa Dodoma linawanyong’onyesha wengi kwa kushindwa kujikita katika taratibu na desturi nzuri za Kitanzania za kujenga umoja, mshikamano na kuvumiliana katika mambo yetu mbalimbali,”amesema Padre Mwaja.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post