» » » ‘Acheni kushirikiana na wauaji’

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge,
Dodoma. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera, Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu, Jenista Mhagama amewataka wafanyakazi wa majumbani kutoshirikiana na wauaji wanaovizia kuwatoa uhai waajiri wao.

Mhagama ametoa kauli hiyo kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi wa majumbani kimataifa yaliyofanyika kitaifa mjini Dodoma.

Amesema kuna baadhi ya wafanyakazi ambao wamekuwa chanzo cha mauaji ya waajiri wao kwa kuwa wamekuwa wakishirikiana na wauaji katika kuyatekeleza.

“Nataka niwaambie jambo moja, mnapokuwa mnafanya kazi hakikisheni kuwa mnazingatia kanuni na sheria za ajira ambazo zinawalinda na siyo kwenda kuiba, kuua au kushirikiana na wauaji katika kuwaua waajiri wenu,” amesema Mhagama.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post