» » Baba adaiwa kumbaka mtoto wake wa miaka mitatu

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


 


Shinyanga. Jeshi la polisi wilayani Kishapu mkoani Shinyanga linamshikilia mtu mmoja mkazi wa kijiji cha Masagala kata ya Maganzo wilayani Kishapu, kwa kosa la kumbaka mtoto wake wa miaka mitatu na kumsababishia maumivu makali sehemu za siri.
Mkuu wa kituo cha polisi Magazo, Osca Shani alisema tukio hilo lilitokea Juni 7, mwaka huu na kwamba baada ya mtoto kufikishwa kwenye kituo cha afya alibainika kufanyiwa kitendo hicho cha kikatili.
“Tunamshikilia mtuhumiwa kwa kosa la kubaka na kumsababisha maumivu makali mtoto wake na kamba atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka,” alisema Shani.
 Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Hawa Ng’humbi alivitaka vyombo vya dola kutoichezea kesi hiyo na kwamba mtuhumiwa afikishwe mahakamani hata na kufungwa jela ili kuondoa matatizo ya ubakaji kwenye wilaya hiyo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post