Naibu Spika wa bunge la Jamhuri Muungano wa Tanzania Mh Dk. Tulia Ackson amesema ipo haja ya kurekebisha sheria na kanuni za uendesaji wa bunge kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila mbunge analipwa posho baada ya kutekeleza majukumu yake ipasavyo na siyo kujisajili kwa lengo la kupata posho na kisha kutoka nje bila ya kutekeleza majukumu yake ya kikatiba.
Mh .Tulia ameyasema hayo alipokuwa akitolea ufafanuzi miongozomiwili iliyowasilishwa bungeni hapo na baadhi ya wabunge akiwemo Mh Dk. Harison Mwakyembe ambaye ni waziri wa katiba na sheria aliyetaka kujua uhalali wa wabunge wa upinzani kuendelea kulipwa posho na mishahra wakati kila kikao kikiongozwa na Naibu Spika wamekuwa wakitoka nje.
Pendekezo hilo la Naibu Spika la kurekebishwa kwa sheria linaungwa mkono na mbunge wa Mkuranga Mh. Abdalah Ulega ambaye anasema ni vyema sheria zibadilishwe ili kurudisha heshima kwa kiti kwani kitendo kinachofanywa na wapinzani kwa siyo cha kiungwana.
Peter Msingwa ni mbunge kutoka Chama Cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA ambaye anasema bunge linaongozwa kwa misingi ya sheria na kanuni na siyo kweli kuwa mbunge katika kutekeleza majukumu yake ni lazima aingie bungeni zipo kazi nyingi za kibunge zinafanyika nje ya ukumbi wa bunge.
Awali katika kipindi cha maswali na majibu mawaziri na manaibu mawaziri walipata nafasi ya kujibu maswali mbalimbali ya wabunge ambapo maswali ya wabunge kutoka kambi upinzani yaliulizwa na wabunge wa CCM ambapo masuala kama changamoto za maji majimboni hayakukosekana.
Mh .Tulia ameyasema hayo alipokuwa akitolea ufafanuzi miongozomiwili iliyowasilishwa bungeni hapo na baadhi ya wabunge akiwemo Mh Dk. Harison Mwakyembe ambaye ni waziri wa katiba na sheria aliyetaka kujua uhalali wa wabunge wa upinzani kuendelea kulipwa posho na mishahra wakati kila kikao kikiongozwa na Naibu Spika wamekuwa wakitoka nje.
Pendekezo hilo la Naibu Spika la kurekebishwa kwa sheria linaungwa mkono na mbunge wa Mkuranga Mh. Abdalah Ulega ambaye anasema ni vyema sheria zibadilishwe ili kurudisha heshima kwa kiti kwani kitendo kinachofanywa na wapinzani kwa siyo cha kiungwana.
Peter Msingwa ni mbunge kutoka Chama Cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA ambaye anasema bunge linaongozwa kwa misingi ya sheria na kanuni na siyo kweli kuwa mbunge katika kutekeleza majukumu yake ni lazima aingie bungeni zipo kazi nyingi za kibunge zinafanyika nje ya ukumbi wa bunge.
Awali katika kipindi cha maswali na majibu mawaziri na manaibu mawaziri walipata nafasi ya kujibu maswali mbalimbali ya wabunge ambapo maswali ya wabunge kutoka kambi upinzani yaliulizwa na wabunge wa CCM ambapo masuala kama changamoto za maji majimboni hayakukosekana.
