Kanisa la Sinza Christian Center limetupiwa nje vyombo vyake nje
kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kutokana na kanisa hilo kudaiwa deni la
zaidi ya Sh. milioni 100. Aliyetekeleza agizo hilo leo ni dalali
aliyepewa tenda hiyo Bw. Joshua ambaye aliteuliwa na Mahakama na jmiliki
wa jengo hilo Bw. Prosper Rwendera.
Akizungumza wakati wa hamisha hamisha hiyo, mke wa mmiliki wa jengo
hilo, Bi. Patricia Prosper alisema; “Huyu aliyepanga hapa hakufuata
utaratibu wowote na ndiyo maana tukapewa jengo letu.”
Alipotafutwa msemaji wa Kanisa ambaye ni Askofu anayedaiwa kuvamia jengo
hilo, hakupatikana kuzungumzia sakata hilo na hata waumini wa kanisa
hilo walipotafutwa walikataa kwa madai hawana mamlaka ya kuzungumzia
lolote kuhusiana na sakata hilo.
Magari yakiwa yanatolewa nje
Kushoto kwa mbali ni Mke wa Miiliki wa Jengo hilo Bi. Patricia Prosper akiendelea na majukumu huku pembeni vijana wakipata maelekezo ya kuendelea kutoa vitu.
Hili ni eneo la Kanisa hilo.
Viti vyote vikiwa vimetolewa nje.
Vitu vikiwa nje ya Jengo hilo ambapo mpaka sasa kuna sinto fahamu vinapelekwa wapi.
Vikombe nje.
Vifaa vikiwa vimetolewa nje.
Wametoa vitu vyote.
Magodoro na vitanda vyote nje.
Source: Global Publisher










