» » BREAKING NEWZZZ….Majambazi wamevamia duka la kubadilishia fedha za kigeni na kupora shilingi milioni 100

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO




Watu wasiojulikana wamevamia duka la Chase Bureau De Change linalotoa huduma ya kubadilisha fedha za kigeni, mali ya Ashraff Khan na kuiba milioni 100 huko wilayani Moshi.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana, baada ya wezi hao kuvunja dirisha la chuma na kuingia sehemu ya kutunzia fedha na kufanikiwa kuiba shilingi za Tanzania, Kenya, na Euro (jumla milioni 100), huku mlinzi wa zamu wa duka hilo akitoweka na kuelekea kusikojulikana.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo jana, huku akitoa taarifa za kuwepo kwa wizi kama huo dukani hapo mwaka 2005, ambapo amesema watu wenye silaha walivamia duka hilo na kupora milioni 44 mchana wa saa sita.
Aidha, kamanda Mutafungwa, amebainisha kuwa, uchunguzi wa awali unaonesha kuwepo kwa dalili za njama za ndani zinazojumuisha kutoonekana kwa mlinzi sehemu ya tukio, huku akiongeza kuwa uchunguzi bado unaendelea dhidi ya tukio hilo.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post