» » Agomea kinga akidai hajawahi kutumia dawa za hospitali

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Serengeti. Mwanafunzi wa darasa la sita Shule ya Msingi Mapinduzi, wilyani hapa, Mkoa wa Mara. Rehema Samson amegoma  kunywa dawa ya kinga inayotolewa bure kwa wanafunzi kwa ajili ya magonjwa yaliyosahaulika (kichocho na minyoo) kwa madai hajawahi kutumia dawa za hospitali toka azaliwe.

Baadhi ya wazazi inadaiwa wamewazua watoto wao wasipokee kinga hiyo inayotolewa bure na Serikali kwamba ni ya Freemason. Imani hiyo imekwamisha mpango huo.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Mapinduzi B’, Obwana Tom alikiri kuwa siku ambayo dawa hizo zilitolewa, mahudhurio ya wanafunzi yalishuka.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post