» » TANESCO yakwama kufanya shughuli zake kwa kuzidai Taasisi za Serikali na Binafsi zaidi ya Milioni Miasita.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Shirika la ugavi wa umeme tanzania (TANESCO) mkoa wa Lindi,linakwama kufanya shughuli zake kwa ufanisi kutokana na kuzidai taasisi za serikali pamoja na watu binafsi zaidi ya shilingi Milioni Miasita.
Akizungumza na waandishi wa habari mbele ya mkuu wa mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi, meneja wa TANESCO, mkoani Lindi,Johnson Mwigune, amesema taasisi za serikali zinadaiwa zaidi ya shilinigi milioni mia tano, huku watu binafsi wakiwa wanadaiwa zaidi ya shilingi milioni sabini.
 
Amesema deni hilo ni la mwisho wa mwezi huu, huku akisisitiza ili shirika liweze kujiendesha na kufanya huduma za kimaendeleo ikiwa ni pamoja na kusambaza umeme katika maeneo yenye maitaji   linakwama kutokana na  fedha nyingi kuwa mikononi mwa taasisi za serikali.
 
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi ameomba taasisi za serikali na watu binafsi,  kulipa fedha hizo kwa wakati ili shirika hilo liweze kujiendesha.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post