» » Mwenge kuzindua miradi 22 Dar

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
Dar es Salaam. Mwenge wa Uhuru ulioingia jijini jana ukitokea Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar unatarajiwa kuzindua miradi 22 ya maendeleo yenye thamani ya Sh19.9 bilioni.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ndiye aliyeupokea Mwenge na baadaye kuanza mbio zake katika Wilaya ya Kinondoni.
Mwenge huo ulipokewa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, mameya pamoja na viongozi wengine wa Serikali na vyama.
Mwenge huo ulikabidhiwa kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando kutoka kwa Katibu Tawala wa Mjini Magharibi, Juma Ally na baadaye Mmbando alimkabidhi Makonda.
Baada ya kukabidhiwa, Makonda alisema utatumika kikamilifu kuhimiza kaulimbiu ulizobeba na kuzindua miradi ya maendeleo katika mkoa wake baada ya hapo akamkabidhi mwenge huo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi kwa ajili ya kuanza rasmi mbio hizo Dar es salaam.
“Kuna miradi 22 itapitiwa na Mwenge; mingine imekamilika, mingine haijakamika ambapo sita itazinduliwa, mitatu itatembelewa, tisa itawekewa jiwe la msingi na minne itafunguliwa. Yote ikiwa na thamani ya Sh19.9 bilioni”, alisema Makonda.
Katika Wilaya ya Kinondoni, Mwenge utatumika kuzindua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya Sh3.2 bilioni ambayo ni Soko la Mburahati, ujenzi wa barabara ya Arsenal Magoti, ujenzi wa wodi ya wajawazito, ujenzi wa Mabweni Mbopo, ujenzi wa kalavati Mabwepande, ujenzi wa Kituo cha Kilimo Malolo na ujenzi wa kisima cha maji Makongo.
Kiongozi wa mbio za Mwenge, George Mbijima aliwataka wananchi kuzingatia ujumbe unaobebwa na Mwenge kwani huangazia masuala muhimu yanayoligusa Taifa kwa wakati huo.
“Mbio za Mwenge mwaka huu zimebeba kaulimbiu isemayo: Vijana ni nguvu kazi ya Taifa washirikishwe na wawezeshwe pamoja na ujumbe wa kudumu kuhimiza mapambano dhidi ya Ukimwi, dawa za kulevya, rushwa na malaria,” alisema Mbijima.
Leo Mwenge utafanya ziara zake Wilaya ya Ilala na kesho utakuwa Temeke kabla ya keshokutwa kuendelea na ziara yake mkoani Pwani.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post