ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Mugabe asema haondoki madarakani.
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kuwa yeye sio Mmarekani wala
Muingereza wakati akiwahutubia karibu watu 50,000, wafuasi wake kwenye
mkutano uliofanyika kwenye mji mkuu Harare kwa heshima yake.
Mugabe mwenye umri wa miaka 92 amekana uwezekano wowote wa kuondoka
madaraklani na kuwashambulia viongozi hasimu ndani ya chama tawala cha
ZANU-PAFU kwa kupanga kumrithi.
Amesema kuwa yeye anawahudumia watu wa Zimbabwe na kuwa ataondoka tu
ikiwa watu wangetaka afanye hivyo. Hata hivyo amesema kuwa haondoki na
haendi popote.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO