» » Moi yaelemewa majeruhi bodaboda

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Madaktari wakimfanyia upasuaji mgonjwa katika

Dar es Salaam. Uhaba wa vifaatiba ni changamoto kwa Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (Moi) kutokana na ongezeko kubwa la majeruhi wa ajali za bodaboda waliolazwa kwa matibabu, imeelezwa.
Ilielezwa kuwa mtu mmoja aliyevunjika kutokana na ajali hiyo, huhitaji vifaatiba vya watu zaidi ya watano.
Akizungumza katika mahojiano na gazeti hili jana, Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Mifupa na Magonjwa ya Ajali wa Moi, Dk Kennedy Nchimbi alisema ongezeko la majeruhi hao limesababisha uhaba wa vifaatiba katika taasisi hiyo kwa sasa.
Dk Nchimbi alisema mwaka 2010 majeruhi wa bodaboda kwa upande wa madereva walikuwa 887, abiria 218 na watembea kwa miguu 254.
Alisema kwa mwaka 2015, idadi ya madereva walioapata ajali za bodaboda iliongezeka hadi kufikia 1,013, abiria 954, waliogongwa 401 na kufanya idadi yao kuwa 2,268 kwa kipindi cha mwaka mmoja. “Ieleweke hawa ni wale ambao hufanyiwa upasuaji wa mifupa hapa Moi, idadi hiyo hatujajumlisha na wale ambao hupatiwa matibabu ya kawaida ambao hufikishwa katika kitengo hiki baada ya kupata ajali,” alisema Dk Nchimbi.
Alisema licha ya ongezeko hilo kutishia usalama wa usafiri wa bodaboda nchini, kwa sasa kuna changamoto nyingine ya kupata mifupa mbadala hasa ya nyonga na goti. Alisema mfupa wa nyonga umekuwa na gharama kubwa ambayo hufikia hadi Sh12 milioni kwa mmoja.
Dk NChimbi alisema pia, kuna upungufu wa mashine za kupumulia majeruhi ambao hali zao ni mbaya baada ya kupata ajali.
Vilevile, alisema taasisi hiyo ambayo imefanya upasuaji wa mifupa kwa watu 55,341 kwa kipindi cha miaka mitano, imekuwa ikielemewa hasa katika upande wa chumba cha upasuaji wa dharura.
Majeruhi wa ajali ya bodaboda, Aisha Milanzi (17) aliyelazwa hospitalini hapo baada ya kupata ajali usiku wa Mei 22 kwa matibabu ya nyonga na mguu wa kulia, alisema walikuwa wamepakizwa mshkaki na dereva mwenye miaka 17.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post