Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya hakimu mkazi–Moshi,Joachim Tiganga amesema mfanyabishara huyo ametiwa hatiani kwa kosa la kuiga nembo ya kampuni ya Mega Trade Investment ya jijini Arusha inayotengeneza vileo aina ya Kiroba orginal.
Mfanyabishara huyo alikamatwa mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita,ambapo alikuwa anatafutwa kwa muda mrefu kutumikia kifungo hicho ambacho hukumu yake ilikuwa imeshatolewa wakati akiwa hayupo mahakamani.
Kesi hiyo ya jinai namba 186 ya mwaka 2012,ilifunguliwa na Jamuhuri katika Mahakama hiyo June 30 baada ya mshtakiwa huyo kukamatwa katika wilaya ya Moshi.
