» » Mfanyabiashara ahukumiwa miaka 5 jela kwa kuiba malighafi ya kutengenezea vileo Moshi.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mfanyabiashara maarufu wa mikoa ya Arusha na Singida,Jonathan Njamas amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela,baada ya kupatikana na hatia katika kosa la wizi wa mali ghafi ya kutengeneza vileo,yenye thamani ya shilingi milioni moja,mali ya kampuni ya Mega Trade Investment ya jijini Arusha

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya hakimu mkazi–Moshi,Joachim Tiganga amesema mfanyabishara huyo ametiwa hatiani kwa kosa la kuiga nembo ya kampuni ya Mega Trade Investment ya jijini Arusha inayotengeneza vileo aina ya Kiroba orginal.

Mfanyabishara huyo alikamatwa mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita,ambapo alikuwa anatafutwa kwa muda mrefu kutumikia kifungo hicho ambacho hukumu yake ilikuwa imeshatolewa  wakati akiwa hayupo mahakamani.

Kesi hiyo ya jinai namba 186 ya mwaka 2012,ilifunguliwa na Jamuhuri katika Mahakama hiyo June 30 baada ya mshtakiwa huyo kukamatwa katika wilaya ya Moshi.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post