"Band kwa sasa haaitwi tena Machozi Band, inatwa The Band, nilibadilisha miaka miwili iliyopita na kwasababu sasa hivi mwenyewe sikutaka kuitwa binti machozi, watu wanasema jina unaloitwa linarelate na maisha yako, so nikaamua kubadili, kwa hiyo Machozi Band haipo tena imekufa, kwa sasa itakuwa ni lady jaydee and the band", alisema Jay dee.
Jaydee ambaye mwisho wa wiki hii anayatajia kufanya tamasha kubwa la 'Naamka tena', amesema tamasha hilo litakuwa ni la masaa matatu bila kupumzika, kwani ana nyimbo zaidi ya 100 ambazo zinaweza zikamfanya afanye show zaidi ya masaa matatu.
