» »Unlabelled » Wasuluhishi waahirisha kwenda Gambia

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO
Rais Yahya Jammeh, akiwa na viongozi wa nchi za Afrika magharibi

Wasuluhishi kutoka maeneo mbalimbali wanaojaribu kutatua mgogoro wa kisiasa nchini Gambia wameahirisha kwenda nchini humo kutokana na ombi la rais Yahya Jammeh.

Badala yake watakwenda nchini humo siku ya Ijumaa.

Viongozi wa nchi za Afrika Magharibi wamemtaka Jammeh akubali kushindwa katika uchaguzi uliofanyika mwezi jana, na kuongeza kusema watahudhuria sherehe za kuapishwa kwa kiongozi wa upinzani Adama Barrow baadae mwezi huu.

Mwanzoni, waziri wa habari za Gambia amesema itakuwa kinyume cha katiba kumwapisha Barrow mpaka pale kesi iliyowakilishwa mahakama na bwana Jammeh ya kupinga matokeo itakapoamuliwa.

Kwa upande mwengine, mahakama kuu nchini humo haitaweza kusikiliza kesi hiyo mpaka mwezi Mei mwaka huu, kutokana na ukosefu wa mahakimu.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post