Fredy Swai (kushoto) na Kanumba enzi za uhai wake. |
Kumekuwa na tatizo kubwa katika mfumo mzima wa uandaaji wa filamu hapa
Tanzania hasa katika suala la kuandaa wasanii ili kuleta uhalisia wa
kazi husika.
…Baada ya kuumizwa.
Kiajana aliyetambuishwa na mama wa aliyekuwa nguli wa filamu hapa
nchini, Steven Kanumba, Flora Mtegoa kuwa ndiye mrithi wa mwanane huyo
kwenye tasnia ya uigizaji, Fred Swai amekumbwa na balaa ambalo ameeleza
kuwa hatolisahau katika maisha yake baada kuunguzwa vibaya na kemikali
usoni katika harakati za kuandaa filamu.
Akizungumza kwenye Kipindi maalum cha Exclusive Interview kupitia Global
TV Online, Swai amesema kuwa siku hiyo aliitwa kwenda kucheza kipande
cha muvi ambacho alitakiwa aigize kama mgonjwa.
Jeraha la Fredy.
Hivyo muandaaji alimtaja afungwe bandeji usoni ili kuonesha uhalisia wa
mgonjwa, ambapo bandeji hiyo ililowanishwa na kemikali zinazotumika
kusafishia vidonda, iodine solution.
Swai aliendelea kueleza kuwa, badala ya kulowanishiwa iodine ya kawaida
isiyo kali (diluted solution) aliwekewa concentrated iodine ambayo ni
kali zaidi hivyo kuunguza sehemu ya paji la uso.
Hii imekuja ikiwa ni siku chache tu baada ya Muigizaji wa Nigeria, Kuchomwa Moto wakati wakishuti video.