» »Unlabelled » Waziri wa Mkapa ataka Magufuli aifumue CCM

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Tuesday, December 13, 2016

Tokeo la picha la magufuli dodoma

Waziri wa zamani wa Serikali ya Awamu ya Tatu, William Kusila (72) amemshauri mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kukifumua chama hicho ili akisuke upya kwa lengo la kukirudisha kwenye misingi yake.



William Kusila


Kusila alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika kijijini kwake Mtitaa, Kata ya Mtitaa wilayani Bahi, takriban kilomita 57 kutoka mjini Dodoma.

Kusila alisema hayo wakati CCM ikielekea kufanya mkutano wa Halmashauri Kuu, ambayo ni chombo cha pili cha juu cha uamuzi baada ya Mkutano Mkuu.

“CCM kilishakuwa kichafu, kilikuwa kichaka cha wala rushwa, wezi, majambazi, wauza dawa ilimradi tu mtu yeyote aliyekuwa na matatizo yake, kimbilio lake lilikuwa ni CCM,” alisema.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post