» »Unlabelled » Abiria wanaosafiri kwenda mikoani wakitokea jijini Dar es salaam wamelalamikia uchache wa mabasi

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Abiria wanaosafiri kwenda mikoani wakitokea jijini Dar es salaam wamelalamikia uchache wa mabasi yanayotoa huduma ya kusafirisha abiria katika kituo cha mabasi ya Ubungo hali ambayo inadaiwa kusababishwa na wingi wa watu wanaosafiri katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu za Krismas na mwaka mpya na kupelekea baadhi ya abiria kushinda kituoni hapo kuanzia asubuhi hadi jioni wakisaka huduma hiyo kwa ajili ya safari.

Wakizungumza na Camera ya Channel Ten iliyofika kituoni hapo kwa ajili ya kujionea hali halisi ya ya Usafiri kwa mabasi yaendayo mikoani abiria hao wamesema kuwa kama ilivyo kwa misimu mingine ya sikukuu kwa miaka iliyopita msimu huu pia hali ya usafiri ni ngumu kutokana na mabasi mengi kusheheni abiria huku abiria wengine wakishindwa kupata nafasi za kusafiri kutokana na ongezeko kubwa la abiria ambapo pia nauli zanadaiwa kupanda kwa baadhi ya mabasi huku mabasi mengine nauli zikibaki kama zilivyokuwa hapo awali…

Licha ya changamoto ya uchache wa Mabasi yaendayo mikoani pia Abiria hao wamelalamiikia uongozi wa kituo hicho kwa kutoweka sehemu za kupumzikia abiria wakati wa kusubiria usafiri wa mabasi licha ya kutozwa ushuru wakati wa kuingia kituoni hapo.


ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Mashak

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post