» »Unlabelled » Wanachama Yanga Wanusurika Katika Ajali Mbaya Ya Gari Wakiwa Njiaji Kuifuata Mbeya City

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Baadhi ya wanachama wa Yanga, wamepata ajali mbaya ya gari.

Bahati nzuri, wote wamefanikiwa kutoka salama katika ajali hiyo iliyotokea katika eneo la Mwidu, wakiwa njiani kwenda Mbeya kuiwahi mechi kati ya Yanga dhidi ya Mbeya City, kesho.

 Baadhi ya viongozi waliokuwa katika gari hilo dogo aina ya Suzuki Vitara ni kamati ya mashindano na ya Utendaji ya Yanga, Omary Said, Bakili Makele na Seif Chuma walikuwa ndani ya gari hilo.

 Makele amethibitisha wao kupata ajali hiyo na kusema wameamua kuahirisha safari.
“Tunashukuru Mungu sana, tumetoka salama ingawa ajali ilikuwa mbaya sana. Sasa tunarejea Chalinze ambako tutafanya taratibu nyingine,” alisema.

Muungwana Blog, inatoa pole kwa wanamichezo hao kwa ajali mbaya iliyowakuta. Mungu awape nguvu zaidi.


ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post