» »Unlabelled » Mr. Blue: Sijawahi kupata tuzo tangu nianze muziki

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Msanii MR. Blue aliyeshika Mic akiwa pamoja na Abby Skills waliposhiriki FNL

Msanii wa Bongo Fleva nchini Mr. Blue ameweka bayana kwamba pamoj na kukubalika na mashabiki wengi na na kuwa kwenye tasnia ya muziki kwa muda mrefu hajawahi kupata tuzo hata moja ya kutambua mchango wake kwenye muziki.

Akizungumza katika kipindi cha Friday Night Live (FNL) kinachorushwa na EATV kila siku ya Ijumaa, Mr. Blue amesema  anatambua umuhimu wa msanii kupata tuzo ila kwa bahati mbaya yeye hajawahi kupata tuzo.

“Mimi sijawahi kupata tuzo yoyote siyo ya kitaifa wala ya kimataifa ila ninachoamini mimi ni kwamba mimi ni ‘expensive’ na ndiyo maana natoa ngoma mara moja kwa mwaka na inadumu kwa muda mrefu” Amesema Mr. Blue

Aidha Mr. Blue ameongeza kuwa tuzo ambazo zimeanzishwa na EATV zitasaidia sana wasanii wengi kuweza kutambulika zaidi na anaamini pengine anaweza kupata tuzo hiyo na ikawa tuzo yake ya mara ya kwanza.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post