» »Unlabelled » Majaliwa awataka waislamu kuhubiri msingi wa dini hiyo

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Waziri mkuu Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa waumini wa dini ya kiislamu nchini kutumia sehemu za ibada kuhubiri masuala ya Mungu na sio siasa .

Waziri mkuu ametoa wito huo aliposhiriki sala ya Ijumaa katika msikiti wa Nunge mjini Dodoma na kuwataka waumini wa dini ya Kiislamu kutumia nyumba ya ibada kuhubiri msingi wa dini.

“Niendelee kusisitiza kwamba wote lazima tutumie muda wetu pamoja na mambo mengine lakini pia tumtafute Mungu kupitia nyumba za ibada. Ndugu waislamu wenzangu tufanye kazi ya kuujenga uislamu wetu kwa kuhakikisha kwamba nyumba hizi za dini kuhubiri uislamu,” alisema.

“Kuhubiri msingi wa dini lakini kusisitiza mshikamano miongoni mwetu kuhakikisha kwamba sisi na majirani zetu tunaishi kwa amani na utulivu, ni jukumu letu muhimu sana.”

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post