» »Unlabelled » Guardiola: Barcelona ni ''mashine''

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

 Barcelona ni ''mashine'' ambayo huenda ikatawala mechi dhidi ya Manchester City siku ya jumatano ,kulingana na Pep Guardiola.raia huyo wa Uhispania alishinda kombe la Ulaya akiwa mchezaji na kocha wakati alipokuwa akiiongoza timu hiyo la La Liga.

Ataelekea tena Nou Camp katika mechi ya vilabu bingwa Ulaya wiki ijayo akijua kibarua kigumu kinachoisubiri timu yake.

''Barcelona ni timu maalum kutokana na mchezo wao,Ni mashine'',alisema.

''Itachukua muda mrefu kuweza kufikia kiwango cha Barcelona,Muongo mmoja uliopita,miaka 50 iliopita Barcelona imekuwa ikitawala katika soka'' .

''Napenda wanavyocheza'',aliongezea.''Wana wachezaji watatu wazuri sana -lionel Messi,Luis Suarez na Neymar mbele.ni washambuliaji hatari.Wana timu nzuri''.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post