» »Unlabelled » Faraja Nyalandu amkingia kifua Miss Tanzania

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

Aliyewahi kuwa Miss Tanzania, Faraja Nyalandu amemkingia kifua mshindi wa mwaka huu Diana Edward akisema hata yeye aliposhinda alizushiwa mambo mengi, lakini anashukuru kwa kuwa yalimjenga.

Katika waraka wake wenye maneno 223 aliouweka kwenye mtandao wa Instagram, mrembo huyo alisema alikaribishwa katika dunia ya umaarufu kwa kashfa lakini kwa msaada wazazi wake alifanikiwa kusimamia malengo yake.

Alimtaka Miss Tanzania afanye anachokiamini na kupuuzia maneno ya watu kwa sababu yanaweza kumtoa katika njia yake.

“Njia ya mafanikio ni ngumu, kwako Miss Tanzania wetu fanya kile unachokiamini, usikubali maneno haya ya watu yakuondoe katika mstari, kwa Watanzania wenzangu tujitahidi kuyaunga mkono yaliyo mazuri, tusibomoe…Tujenge,” alisema.

Akizungumzia ushindi wake, Diana alisema amejipanga kulitumikia vyema hasa kukomesha vitendo vya ukeketaji katika jamii ya Kimasai.

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post