» »Unlabelled » Bei ya mafuta yavunja bunge, mawaziri wote wajiuzulu

ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO


Mgogoro wa bei ya mafuta wasababisha bunge la kuwait kuvunjwa
Baraza la mawaziri la Kuwait limejiuzulu huku bunge likivunjwa na hivyobasi kuitisha uchaguzi mpya.
Hatua hiyo inafuatia mgogoro kati ya wabunge na serikali kufuatia kupandishwa kwa bei ya mafuta katika taifa hilo lenye utajiri mkubwa wa mafuta.
Runinga ya taifa imesema kuwa ukosefu wa ushirikiano ndio sababu ya tukio hilo.
Huku bei ya mafuta kote duniani ikisalia kuwa ya chini ,serikali ya Kuwait imepunguza baadhi ya faida ikiwemo ruzuku ya mafuta na kupandishwa kwa bei ya petroli hadi asilimia 80.
Hili lilizua pingamizi.Serikali ilitarajiwa kumaliza muda wake wa miaka minne ifikiapo Julai mwaka ujao.
Wabunge katika bunge la sasa wanadhaniwa kuunga mkono serikali lakini wamewasilisha maombi matatu ya kuwahoji mawaziri kuhusu bei hizo mpya.
Baada ya mkutano wa dharura uliotishwa na serikali siku ya Jumapili jioni,Amir wa Kuwait Sheikh Sabah al-Ahmad al Sabah,alitoa amri ya kulivunja bunge kutokana na hali ilivyo katika eneo hilo.
Runinga ya taifa ilitangaza kuwa mawaziri wote wamejiuzulu.
ILI UPATE HABARI ZETU KWA URAHISI BOFYA HAPA KUINSTAL APPLICATION YA MZALENDO HURU KWENYE SIMU YAKO

About Unknown

About Mzalendo Huru Staff:

Send us your articles, questions, feedback, suggestions, press releases and all others to Whats app on +255657905751
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post